Mar 15, 2013

BOEING 787 THE DREAMLINER KURUDI KAZINI.

The Dreamliner!
    Kampuni ya kutengeneza ndege za kibiashara ya Boeing,ilipata kibali cha kufanya safari za majaribio kwa ajili ya ndege yao mpya ya Boeing 787 The Dreamliner juzi tarehe 13 kutoka FAA (Federal Aviation Administration) Marekani. Kibali hicho kinakuja baada ya kampuni ya Boeing kutoa designs za betri mpya amabazo zitatumiwa na ndege aina ya Boeing 787.
   FAA iliamuru mashirika yote duniani yaliuyokuwa yakitumia ndege hizo tarehe 2 Januari mwaka huu,baada ya ndege ya shirika la Japan Airlines kupata dharura ikiwa angani. Dharura hiyo ilihusisha betri ya Auxiliary Power Unit kuungua na kuanza kutoa moshi amabo uliingia kwenye chumba cha abiria.
   Boeing imerusha ndege ya kwanza leo katika uwanja wa ndege wa Narita karibu na Tokyo Japan (kama ionekanavyo kwenye picha chini).
Ndege aina ya Boeing 787 ikiwa katika uwanja wa Narita Tokyo kabla ya majaribio.
(Credit:ANA)
   Boeing itakuwa kampuni ya kwanza kutumia betri za aina ya Lithium-ion,ambazo zinatunza zaidi charge kwa muda muda mrefu kuliko aina zingine na zinatumika kwa muda mrefu. Kila betri moja ina seli nane ili kuhakikisha usalama zaidi!
   Pia,zimetengenezwa na kuta maalumu kwa ajili ya kuzuia moto (fireproof shell) au joto la betri moja lisiathiri seli nyingine. Kama majaribio hayo yatafanikiwa,ndege hizo zitarudi kazini ndani ya wiki chache baada ya leo!


3 comments: