Feb 1, 2013

FLY EMIRATES WABADILISHA NDEGE INAYOKUJA DAR ES SALAAM!

Leo ni siku nzuri sana kwa wasafiri waendao Dubai. Shirika la ndege la Umoja wa nchi za Kiarabu (UAE-United Arab Emirates) Fly Emirates,limeanza rasmi kutumia ndege yake aina ya Boeing 777-300ER (Extended Range) kwa safari za kutoka Dar es Salaam kwenda Dubai.
Hapo mwanza ilitumika ndege aina ya Airbus A340-500 yenye uwezo wa kubeba abiria 340.
Ndege hiyo mpya ya Boeing 777-300ER itaweza kubeba abiria 360,abiria 8 katika daraja la kwanza (first class) 24 daraja la kibiashara (business class) na 310 daraja la chini (economy class).
Pia itabeba tani 46 za mizigo.

NAULI ZA SAFARI HIYO
Daraja la chini (economy class) kwenda na kurudi-630$

Daraja la kibiashara (business class) kwenda na kurudi-2,260$.

Ndege hiyo itakuwa ikiondoks Uwanja wa ndege wa Dubai saa 1015hrs na kufika Dar es Salaam saa 1455hrs. Na itaondoka Dar es Salaam saa 1645hrs na kufika Dubai saa 2320hrs
http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=50513