Feb 1, 2013

TAA ZILIZO PEMBENI MWA BARABARA YA KURUKIA NA KUTUA NDEGE..ZINAMAANISHA NINI?

Bila shaka umewahi kuona taa zilizo pembeni mwa barabara
inayotumiwa na ndege kuruka na kutua,sivyo! Umewahi kujiuliza zina kazi gani!
Huenda ulisema "ni kwa ajili ya kumsaidia rubani kuona
mahali ndege yake inatakiwa kutua".

Lakini,taa hizo zina kazi nyingine ya maana sana....!
Ungependa kujua ni nini? Endelea kusoma.

Ndege inapoanza kushuka,inashuka ikiwa na pua yake
(nose) imeanglia chini Lakini katika Angle fulani ambayo
mara zote ni nyuzi tatu (3 degrees).
Taa hizo zinamsaidia rubani kutambua ikiwa ndege yake
inashuka katika angle hiyo inayotakiwa.
Taa hizo zimeundwa kutoa mwanga wa rangi fulani kutokana
na angle ambayo zinaangaliwa.
Zikiangaliwa toka juu sana zinaonekana nyekundu,zikiangaliwa
toka chini kidogo zinaonekana kijani na zikiangaliwa nusu wima(45 Degrees)
zinaonekana nyeupe.

Sasa hebu tuone zinamsaidiaje rubani kujua hilo.

Kanuni ifuatayo inatumika na marubani kujua ikiwa ndege inashuka
katika angle sahihi...

White-white-white-white(yaani upande mmoja nyeupe na wa pili nyeupe)
    ~Ndege ipo kwenye angle sahihi.
White-white-white-red(yaani upande mmoja mbili nyeupe na wa pili nyeupe na nyekundu)
    ~Ndege ipo juu kidogo ya angle sahihi.
White-white-red-red(upande mmoja mbili nyeupe na wa pili mbili nyekundu)
    ~Ndege ipo chini kidogo ya angle sahihi.
Red-red-red-red (pande zote mbili nyekundu)
    ~Ndege ipo chini sana.